I made this widget at MyFlashFetish.com.

code-matuwille

MPENZI MSIKILIZAJI WA MBEYA FM, PENDEKEZA WIMBO UNAOONA UNAFAA KUINGIA KWENYE TOP 30, KABLA YA JUMAPILI AU TUMA MAONI YAKO KUPITIA 0757762963

2011

WAJANJA WA TOWN

WASIKILIZE WAJANJA WA TOWN KUPITIA 89.5 MBEYA FM....PRESENTER-VICE PRESIDENT NA SMART BOY

September 10, 2011

AJALI MBAYA ZANZIBAR., MELI YA SPICE YAZAMA

Meli ya LCT Spice Islanders ikiwa imezama Pwani ya Nungwi.



Meli ya LCT SPICE ISLANDERS imebinuka na kuzama katika Bahari ya Hindi huko Pwani ya Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja ikielekea Pemba.

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu, Mh Issa Haji Ussi akithibitisha tukio hilo amesema ajali  imetokea milango ya saa 8:30 za usiku wa kuamkia leo, na kuongezea kuwa  meli hiyo ilikuwa imebeba abiria 610 pamoja na mizigo.


Mh Ussi  amesema meli hiyo iliyokuwa imeondoka katika Bandari ya Malindi Unguja ikiwa katika hali ya uzima, lakini katikati ya safari ikapata hitilafu na kusababisha kubiruka na hatimaye kuzama.
Hadi sasa haijaweza kufahamika idadi kamili ya watu waliofariki,lakini vyombo vya uokozi vimefika katika eneo la tukio kutoa msaada.

Naibu Waziri  huyo  amesema Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya usafiri vya binafsi  vya boti ziendazo kasi zimekwenda eneo la tukio kutoa msaada unaohitajika, huku Jeshi la Polisi Tanzania limetuma Helikopta yake kwenye eneo la tukio.

Awali, amesema Mamlaka zinazohusika zilipata taarifa za kuzama kwa meli hiyo baada ya Meli ya Mv Jitihada inayomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuripoti kuzama kwa meli ya Spice Islanders ambayo ililazimika kukatisha safari yake kuelekea Kisiwani Pemba na kwenda kwenye tukio.

Serikali imesema taarifa zaidi zitakuwa zikitolewa na wananchi wameombwa kuwa watulivu.

Kwa Habari zaidi endelea kutembelea Mtandao wetu

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni yako hapa chini

TANGAZA NASI KWA BEI NAFUU.., WASILIANA NASI 0757762963

TANGAZA NASI KWA BEI NAFUU.., WASILIANA NASI 0757762963
Matangazo hayo pia yatarushwa moja kwa Moja Kupitia 89.5 MBEYA FM Radio.!!